Aceria guerreronis
Mchwa
Dalili za kwanza za shambulizi ni uwepo wa madoa madogo, ya rangi ya njano iliyopauka ama nyeupe, ya umbo la pembe tatu, ambayo huonekana kwenye matunda machanga sana, kwenye kidaka kinachoyafunika. Kadri matunda yanavyokua, madoa haya hugeuka na kuwa ya rangi ya kahawia ama nyeusi, na kisha gamba la juu huparuza na kutengeneza nyufa kubwa zenye kina kirefu. Kwa kuwa utitiri hawa hupata chakula chao kwenye eneo fulani mahsusi, nazi hukua zikiwa na umbo lisilo sawa, hivyo kuonekana ndogo ama kuumbika vibaya. Mara nyingi, matunda machanga huweza kudondoka kutoka mtini kabla ya wakati. Pindi nazi zinapovunwa, nyama yake ya ndani huwa ndogo sana, na nyuzinyuzi za ganda lake mara nyingi huwa zimeharibika na huwa ngumu kutumika.
Chaguzi zilizopo ni pamoja na kutumia utitiri wazuri wenye manufaa ambao kiasili huwawinda na kuwala utitiri waharibifu waliopo kwenye vidaka vya matunda. Aina fulani za kuvu wasio waharibifu wanaweza pia kutumika; kuvu hawa hukua juu ya utitiri hawa na kisha kuwauwa. Mafuta asilia, kama vile yale yaliyotengenezwa kwa mwarobaini ama kitunguu swaumu, yanaweza kupulizwa kwenye vichane vya matunda vinavyokua ili kuwafukuza utitiri hawa na kukwamisha uwezo wao wa kula chakula. Njia hizi ni fanisi zaidi pindi zinapotumika mapema punde tu matunda ya mwanzo yanapoanza kuumbika.
Daima zingatia kutumia njia mseto zinazojumuisha mbinu za kinga sambamba na tiba za kiasili/zilizo rafiki kwa mazingira. Ni ngumu kuwadhibiti utitiri hawa kwa kutumia vimiminika kwani wao hujificha kwenye mianya membamba iliyopo chini ya kidaka cha tunda. Ili tiba yoyote ile iweze kufanya kazi, lazima tiba hiyo ielekezwe moja kwa moja kwenye "sehemu ya juu" ya mti husika na hasahasa kwenye vichane vya matunda machanga zaidi. Ni vyema zaidi kuchukua hatua mapema mwanzoni mwa msimu ili kuzuia idadi ya utitiri hawa kuongezeka. Ni bora zaidi kutumia njia mbalimbali za udhibiti kuliko kutegemea njia moja pekee, kwani kufanya hivyo kutasaidia kuwazuia utitiri hawa kugeuka kuwa sugu baada ya muda.
Tatizo hili husababishwa na utitiri wadogo sana, wenye umbo la karoti, ambao ni wadogo sana kiasi kwamba hawawezi kuonekana bila kutumia darubini. Utitiri hawa huishi katika jamii kubwa zilizojificha katika kidaka cha tunda la nazi, ambapo hufyonza majimaji yaliyopo kwenye tishu laini ya kidaka hicho. Utitiri hawa hukua upesi, wakizalisha kizazi kipya kila baada ya siku 7 hadi 10, hivyo kuifanya idadi yao kuongezeka haraka. Husambazwa kwa urahisi kutoka mti mmoja kwenda mwingine kupitia upepo, ama husafirishwa na wadudu na ndege. Ingawa utitiri hawa huwa hai kipindi chote cha mwaka, kwa kawaida husababisha madhara makubwa zaidi misimu ya kiangazi ama katika majira yenye unyevunyevu mwingi.

This page is powered by millions of live Plantix diagnoses. See where Utitiri wa Nazi is spreading — district by district — with Crop Insights, part of Plantix Intelligence.