Nazi

Utitiri wa Nazi

Aceria guerreronis

Mchwa

Kwa Ufupi

  • Madoa ya rangi ya njano iliyopauka ama meupe, ya umbo la pembe tatu, huonekana karibu na kidaka cha nazi changa.
  • Madoa haya hugeuka na kuwa ya rangi ya kahawia ama nyeusi na kisha hutengeneza nyufa kubwa, zenye miparuzo.
  • Mara nyingi, nazi zilizoshambuliwa huwa ndogo, husinyaa, na hupoteza umbo lake.
  • Matunda machanga yanaweza kudondoka kutoka kwenye mti kabla hayajawa tayari kuvunwa.
  • Ubora wa nyama ya nazi na nyuzinyuzi za gamba la nazi hupungua kwa kiasi kikubwa.

Inaweza pia kupatikana kwenye

0 Mazao

Nazi

Dalili

Dalili za kwanza za shambulizi ni uwepo wa madoa madogo, ya rangi ya njano iliyopauka ama nyeupe, ya umbo la pembe tatu, ambayo huonekana kwenye matunda machanga sana, kwenye kidaka kinachoyafunika. Kadri matunda yanavyokua, madoa haya hugeuka na kuwa ya rangi ya kahawia ama nyeusi, na kisha gamba la juu huparuza na kutengeneza nyufa kubwa zenye kina kirefu. Kwa kuwa utitiri hawa hupata chakula chao kwenye eneo fulani mahsusi, nazi hukua zikiwa na umbo lisilo sawa, hivyo kuonekana ndogo ama kuumbika vibaya. Mara nyingi, matunda machanga huweza kudondoka kutoka mtini kabla ya wakati. Pindi nazi zinapovunwa, nyama yake ya ndani huwa ndogo sana, na nyuzinyuzi za ganda lake mara nyingi huwa zimeharibika na huwa ngumu kutumika.

Mapendekezo

Udhibiti wa Kiasili

Chaguzi zilizopo ni pamoja na kutumia utitiri wazuri wenye manufaa ambao kiasili huwawinda na kuwala utitiri waharibifu waliopo kwenye vidaka vya matunda. Aina fulani za kuvu wasio waharibifu wanaweza pia kutumika; kuvu hawa hukua juu ya utitiri hawa na kisha kuwauwa. Mafuta asilia, kama vile yale yaliyotengenezwa kwa mwarobaini ama kitunguu swaumu, yanaweza kupulizwa kwenye vichane vya matunda vinavyokua ili kuwafukuza utitiri hawa na kukwamisha uwezo wao wa kula chakula. Njia hizi ni fanisi zaidi pindi zinapotumika mapema punde tu matunda ya mwanzo yanapoanza kuumbika.

Udhibiti wa Kemikali

Daima zingatia kutumia njia mseto zinazojumuisha mbinu za kinga sambamba na tiba za kiasili/zilizo rafiki kwa mazingira. Ni ngumu kuwadhibiti utitiri hawa kwa kutumia vimiminika kwani wao hujificha kwenye mianya membamba iliyopo chini ya kidaka cha tunda. Ili tiba yoyote ile iweze kufanya kazi, lazima tiba hiyo ielekezwe moja kwa moja kwenye "sehemu ya juu" ya mti husika na hasahasa kwenye vichane vya matunda machanga zaidi. Ni vyema zaidi kuchukua hatua mapema mwanzoni mwa msimu ili kuzuia idadi ya utitiri hawa kuongezeka. Ni bora zaidi kutumia njia mbalimbali za udhibiti kuliko kutegemea njia moja pekee, kwani kufanya hivyo kutasaidia kuwazuia utitiri hawa kugeuka kuwa sugu baada ya muda.

Ni nini kilisababisha?

Tatizo hili husababishwa na utitiri wadogo sana, wenye umbo la karoti, ambao ni wadogo sana kiasi kwamba hawawezi kuonekana bila kutumia darubini. Utitiri hawa huishi katika jamii kubwa zilizojificha katika kidaka cha tunda la nazi, ambapo hufyonza majimaji yaliyopo kwenye tishu laini ya kidaka hicho. Utitiri hawa hukua upesi, wakizalisha kizazi kipya kila baada ya siku 7 hadi 10, hivyo kuifanya idadi yao kuongezeka haraka. Husambazwa kwa urahisi kutoka mti mmoja kwenda mwingine kupitia upepo, ama husafirishwa na wadudu na ndege. Ingawa utitiri hawa huwa hai kipindi chote cha mwaka, kwa kawaida husababisha madhara makubwa zaidi misimu ya kiangazi ama katika majira yenye unyevunyevu mwingi.


Hatua za Kuzuia

  • Chagua na otesha nazi za aina mbalimbali zenye ukinzani wa asili kwa utitiri.
  • Ipatie miti lishe kamili, hali ukihakikisha kwamba inapata viwango vya kutosha vya naitrojeni, fosforasi, na potasiamu.
  • Ongeza virutubisho vya ziada kwenye udongo kama vile borax ama gypsum ili kuimarisha kinga asili ya mti.
  • Mwagilia miti vizuri, hasa kipindi cha misimu ya kiangazi, ili kupunguza kukakamaa kwa mmea.
  • Ondoa na teketeza "vifundo" na matunda madogo yote yaliyodondoka.
  • Kufanya hivi husaidia kuondoa hifadhi ambazo utitiri huweza kujificha.
  • Panda miti mirefu ama vizuia upepo kulizunguka shamba ili kuzuia upepo ambao huwabeba utitiri hawa.
  • Otesha mazao yanayorutubisha udongo kama vile marejea.
  • Haya huimarisha udongo na kuwalisha wadudu wenye manufaa.
  • Kagua vichane vya matunda machanga mara kwa mara vilivyopo juu ya mti ili kugundua mapema dalili za uwepo wa manjano.

Pakua Plantix