Kakao

Kuoza kwa Maganda kwa Ukungu Mweupe

Moniliophthora roreri

Kuvu

Kwa Ufupi

  • Maganda huvimba na kupata madoa ya kahawia iliyokolea yanayosambaa haraka.
  • Utando mweupe wa unga huonekana kwenye sehemu zilizoambukizwa.
  • Ndani ya ganda huoza na kuwa na rangi ya kahawia-nyekundu.
  • Maganda yaliyoambukizwa huwa mazito kuliko maganda yenye afya.
  • Hatimaye maganda hukauka na kuwa magumu, meusi, kama mabaki yaliyokauka.

Inaweza pia kupatikana kwenye

0 Mazao

Kakao

Dalili

Kuoza kwa maganda kwa ukungu mweupe huathiri maganda ya kakao katika hatua tofauti, na dalili hubadilika kadri maganda yanavyozeeka. Ugonjwa huu hushambulia maganda na matunda pekee, na hauathiri majani wala matawi. Maganda machanga huonyesha uvimbe juu ya ngozi yake na huwa ya rangi ya njano hafifu. Ndani ya ganda huwa laini na huwa na majimaji. Maganda yanayokua hupatwa na uharibifu na uvimbe mkubwa zaidi, huku madoa makubwa ya kahawia yakitokea na kusambaa kwenye sehemu yote ya juu ya ganda. Sehemu iliyoambukizwa hufunikwa na vimelea vya kuvu vyenye mwonekano wa unga mweupe. Kuiva mapema kunaweza kutokea, na ganda huoza kwa ndani likiwa na mwonekano wa kahawia-nyekundu. Maganda yaliyokomaa hufunikwa na madoa ya kahawia yenye mafuta yasiyo na umbo maalumu, ambayo huungana pamoja na hatimaye kufunikwa na tabaka la unga mweupe. Maganda huonekana mazito na baada ya muda husinyaa, na kuwa magumu, meusi, kama mabaki yaliyokauka.

Mapendekezo

Udhibiti wa Kiasili

Kama ilivyo kwa dawa za kuvu za kikemikali, udhibiti wa kibiolojia hufanya kazi vizuri zaidi unapofanyika kabla maganda hayajaambukizwa. Baadhi ya spishi za Trichoderma zimeonyesha matokeo mazuri katika kudhibiti kuvu huyu, zikitumika mara kwa mara na kwa njia ya kinga.

Udhibiti wa Kemikali

Dawa za kuvu za kikemikali zinaweza kusaidia kudhibiti ugonjwa huu, lakini dawa hizi hufanya kazi vizuri zaidi pindi zinapotumiwa sambamba na mbinu bora za kilimo. Kinga ni bora na nafuu zaidi kuliko kujaribu kutibu miti iliyoambukizwa. Elekeza unyunyiziaji kwenye maganda, hasa maganda machanga. Nyunyizia wakati wa hali ya hewa kavu. Tumia mashine za kunyunyizia zenye mota ili kuyafikia vizuri maganda yote.

Ni nini kilisababisha?

Kuoza kwa maganda kwa ukungu mweupe husababishwa na kuvu Moniliophthora roreri. Maganda machanga yenye umri wa miezi 0–3 ndiyo huathirika zaidi, wakati maganda yaliyokomaa yenye umri wa miezi 5–6 huwa na ukinzani bora zaidi. Vimelea vya kuvu vinaweza kusambazwa na upepo na matone ya mvua yanayoruka, na hupendelea unyevunyevu mwingi, jambo linalofanya msimu wa mvua kuwa kipindi kikuu cha kusambaa kwa ugonjwa. Pia, vifaa vilivyochafuliwa, nguo, na kuhamisha maganda yaliyoambukizwa ndani ya shamba husambaza vimelea hivyo. Mzunguko duni wa hewa kwenye mwavuli mnene wa miti pia ni hali inayochochea ugonjwa.


Hatua za Kuzuia

  • Tumia aina za kakao zenye ukinzani dhidi ya ugonjwa huu pale zinapopatikana.
  • Kagua mimea kila wiki na ondoa mara moja maganda yaliyoambukizwa, hasa maganda machanga.
  • Zika maganda yenye ugonjwa angalau sentimita 50 ardhini au yachome moto.
  • Usisafirishe kamwe maganda kutoka kwenye maeneo yaliyoambukizwa.
  • Pogoa miti mara mbili kwa mwaka ili kuboresha mzunguko wa hewa.
  • Ondoa matawi yanayokutana/yanayogusana na vitawi vilivyochipuka kutoka kwenye shina.
  • Dumisha matawi ya mti katika usao wa chini, takriban urefu wa mita 3–4.
  • Boresha mtiririko wa maji ili kupunguza unyevunyevu.
  • Palilia mara kwa mara ili kuondoa mimea inayoweza kuhifadhi ugonjwa.
  • Vuna maganda yaliyoiva mara kwa mara; usiache matunda yaliyoiva kupita kiasi.
  • Safisha na kuua vijidudu kwenye vifaa vya kazi.

Pakua Plantix