Golovinomyces cichoracearum
Kuvu
Mwanzoni, huonekana kama madoa meupe, ya unga, kwenye sehemu ya juu ya majani yanayoelea chini, yaliyozeeka zaidi. Baada ya muda, madoa haya hupanuka na kufunika eneo zima la jani. Madoa haya ya unga unga yanaweza pia kuonekana kwenye shina na kwenye sehemu za chini za majani, pindi madhara yanapokuwa makali zaidi. Majani yaliyoathirika hugeuka kuwa ya manjano, kisha huwa na rangi ya kahawia, na yanaweza kufa. Mimea iliyoathirika sana inaweza kudhoofika na kuzeeka mapema. Miundo midogo meusi ya mviringo inaweza kutokea ndani ya madoa haya meupe katika hatua za mbeleni za maambukizi.
Nyenzo za kiasili kama vile spishi za Trichoderma na Bacillus subtilis, bidhaa zenye salfa, michanganyiko yenye potasiamu bikaboneti ama vioevu vya mafuta ya mwarobaini vinaweza kusaidia pindi vinapotumiwa mapema.
Daima zingatia kujumuisha njia mseto zinazotumia suluhisho za kinga sambamba na tiba za kiasili ama zilizo rafiki kwa mazingira. Dawa za kuuwa kuvu hufanya kazi vizuri zaidi pindi zinapotumiwa kama kinga ama pindi zinapotumiwa mwanzoni mwa dalili za ugonjwa. Hakikisha matawi yanafikika vizuri wakati unapoyapulizia dawa kwani pathojeni husambaa upesi katika mmea. Badili aina ya dawa za kuvu mara kwa mara ili kupunguza hatari ya mmea kuwa sugu kwa dawa fulani.
Tofauti na magonjwa mengi ya kuvu, ugonjwa huu hustawi katika hali za joto, kavu, zenye kiasi kidogo cha unyevunyevu. Joto la mchana na ubaridi wa usiku huchochea kuenea kwa ugonjwa huu. Husambaa kwa urahisi kupitia hewa. Kuvu huyu haitaji uwepo wa maji kwenye jani ili kuliambukiza. Huendelea kuishi kipindi kisicho cha msimu katika mabaki ya mimea iliyoathirika na kwenye mimea mwitu inayoathiriwa kirahisi na pathojeni kama vile mualizeti mwitu. Matawi mengi yaliyosogeleana, yasiyopitisha hewa vizuri, huchochea hatari ya maambukizi.

This page is powered by millions of live Plantix diagnoses. See where Ubwiri Unga wa Alizeti is spreading — district by district — with Crop Insights, part of Plantix Intelligence.