Alternaria helianthi
Kuvu
Madoa ya rangi ya kahawia yanaweza kuonekana kwenye majani, shina za majani, shina za matawi, sepali, na kwenye petali za mmea. Kuvu huyu husababisha ugonjwa wa mabaka kwenye miche, na uozo wa kishada. Kwenye majani, vidonda hivi huwa vya rangi ya kahawia iliyokolea, vyenye ukingo uliopauka sambamba na mduara wa mwanga wa manjano. Kadri ugonjwa unavyoendelea, ukubwa wa vidonda huongezeka hadi kufikia takribani kipenyo cha sentimita 2-3 na baadaye huungana na kutengeneza kidonda chenye umbo lisilo la kawaida, na kisha kutengeneza baka na mnyauko wa majani. Eneo hizi huzungukwa na kanda ya klorotiki yenye sehemu ya kati iliyooza, ya rangi ya nyeupe ya kijivu. Madoa hujitokeza kwanza kwenye majani ya chini na kisha husambaa kwenye majani ya kati na ya juu. Kwenye mashina, vidonda huonekana kama madoa meusi ya mviringo, marefu ama yenye vifereji. Kwenye sepali na kwenye petali, madoa hufanana na yale yaliyopo kwenye majani, lakini hapa huwa na umbo dogo zaidi (kipenyo cha sentimita 0.5-2) na huchanganyika. Matokeo ya maambukizi haya ni kuibuka kwa mabaka na kupukutika kwa majani, kuharibika kwa maua na vishada vya mbegu, kunyauka kwa mimea, kubabuka kwa shina na hatimaye kufa kwa mmea. Pia, wakati mwingine, vishada vya maua huoza.
Ili kuuchochea udongo kujisafisha wenyewe baada ya mavuno yanayotangulia msimu wa vuli, inapendekezwa kwamba bidhaa za kiasili zenye Trichoderma spp. ama nyenzo za kibiolojia za kudhibiti pathojeni wa mimea (Bacillus spp., Pseudomonas spp.), zitumike.
Daima zingatia matumizi ya njia mseto zinazojumuisha mbinu za kinga sambamba na tiba za kiasili, ikiwa kama zinapatikana. Katika uoteshaji, tumia mbegu zilizotibiwa kwa dawa za kuuwa kuvu zenye imazalil na tebuconazole (dawa za kuuwa kuvu zinazofuata mfumo maalum). Katika kipindi cha kukua kwa mmea, kutumia dawa zenye cymoxanil (dawa ya kuuwa kuvu ifuatayo mfumo maalum), boscalid, na tebuconazole (dawa ya kuuwa kuvu ifuatayo mfumo maalum) kunaweza kudhibiti ugonjwa huu.
Husababishwa na kuvu aitwaye Alternaria helianthi. Pathojeni huyu huishi kwenye mabaki ya mbegu na mimea. Mimea huwa hatarini kupatwa na maambukizi kuanzia kwenye hatua ya kuchipuka hadi kipindi cha mavuno. Ugonjwa huu husambaa kwa kasi katika hali ya hewa ya joto, kavu, yenye mvua zinazonyesha kwa kipindi fulani. Utumiaji kupita kiasi wa mbolea zenye naitrojeni huzidisha uharibifu wa mmea.

This page is powered by millions of live Plantix diagnoses. See where Baka la Alizeti is spreading — district by district — with Crop Insights, part of Plantix Intelligence.