Transpiration disorder
Nyingine
Malengelenge/Viupele vyenye maji na madoa ya njano kwenye upande wa chini wa majani. Hii inaweza kusababisha kujikunja kusiko kwa kawaida kwa majani. Malengelenge hayo yanaweza kutokea kwenye shina na matunda pia. Majani yanaweza kukakamaa na yanaweza kupasuka yanapoguswa. Hii ni kwa sababu malengelenge hudhoofisha muundo wa majani. Ingawa uvimbe wa majani kwa kawaida hauathiri afya ya mmea kwa ujumla, inaweza kufanya mboga isiwe na mvuto sana kwa kuuza, na hivyo kusababisha hasara za kiuchumi. Sehemu zote laini za mazao ya mboga mboga zinaweza kuupata uvimbe wa majani ikiwa hali ya hewa inaruhusu.
JAMBO hili si mdudu wala ugonjwa; kwa hivyo, udhibiti wa kibayolojia hauhitajiki au hauhusiki.
Jambo hili si mdudu wala si ugonjwa; kwa hiyo, udhibiti wa kikemikali hauhitajiki au hauhusiki.
Kumwagilia kupita kiasi, udongo unao tuamisha maji, siku za baridi na mawingu, unyevu mwingi. Uvimbe wa majani hutokea wakati mimea inafyonza maji kwa kasi zaidi kuliko inavyoweza kuyatoa kupitia majani. Mara nyingi hutokana na kumwagilia kupita kiasi siku za mawingu na mwanga hafifu, unyevu wa juu au mzunguko mdogo wa hewa. Kabichi na nyanya huathiriwa sana na hali hii, hasa katika udongo unao tuamisha maji. Malengelenge yanayosababishwa na uvimbe wa majani huendelea kuwepo hata kama hali ya hewa inapo boreka.