Physiological Disorder
Nyingine
Dalili huwa na sifa ya maeneo ya ulalo ya kijani hafifu hadi meupe kwenye pande zote za jani. Mistari iliyobadilika rangi huonekana karibu na sehemu ya chini ya majani ya zamani na hatua kwa hatua kwenye majani machanga mfululizo. Ndani ya shamba, dalili zinaweza kuonekana kwenye mimea tofauti kwa kimo sawa kutoka ardhini. Madoa yaliyokufa na kuchanika huonekana ndani ya mabaka au mikanda ya majani machache yaliyoathirika. Miwa mifupi kwa kawaida haina kasoro hii.
Hadi leo, hatufahamu mbinu yoyote ya udhibiti wa kibayolojia inayopatikana dhidi ya kasoro hii.
Daima zingatia mbinu jumuishi na hatua za kuzuia pamoja na matibabu ya kibayolojia ikiwa yanapatikana. Uharibifu huu hauathiri sana mmea.
Mabadiliko ya rangi yenye mistari ni shida ya kimaumbile ambayo kimsingi husababishwa na kushuka kwa ghafla kwa joto. Ina athiri sehemu za majani yasiyo funguka ndani ya msokoto. Uharibifu kawaida huonekana wiki chache baadaye, wakati majani yanakua, na haiathiri sana mavuno ya mazao na taratibu nyingine. Viwango vya joto kati ya 2.7 na 7 ° C hupelekea kasoro hii. Mashamba katika maeneo ya miinuko yanaathirika zaidi kuliko mashamba ya nyanda za chini. Kasoro hii inaweza pia kusababishwa na joto kwenye baadhi ya aina zenye mshtuko zaidi kwa joto, hasa pale majani yanapojipinda kawaida.