Cletus trigonus
Mdudu
Utaona kunguni/mende wadogo, kahawia hadi kijivu wenye miili bapa na mabega makali yakitoka nyuma ya vichwa vyao. Wadudu hawa hula kwa kunyonya punje changa za mpunga na majani. Kula kwao hutengeneza madoa madogo meusi hasa kwenye punje. Madoa haya yanaweza kuathiri mwonekana na ubora wa mchele.
Sabuni ya kuua wadudu au mimea, kama vile mafuta ya mwarobaini au pareto, vinaweza kutoa udhibiti wa mende wachanga. Kunguni/mende wa majani kama vile kunguni/mende mwembamba wa mpunga, wana maadui wengi wa asili, wakiwemo ndege, buibui na wadudu wanaowawinda na kuwanyonya. Ili kusaidia kudhibiti mende/kunguni wa majani, unaweza kuvutia maadui hawa wa asili kwa kutoa makazi na maji kwa ndege na kutumia dawa chache za wigo mpana.
Mdudu huyu anachukuliwa kuwa ni mdudu wa kwenye majani. Kwajili ya mende wa majani kuna aina mbalimbali za dawa za kuulia wadudu hao. Wadudu hawa wangeweza kuruka mbali ikiwa watasumbuliwa na wanaweza kutoroka kutoka kwa mimea wakati wa kunyunyiza dawa; hivyo, ni bora kunyunyiza asubuhi na mapema wakati wakiruka/kutembea polepole kutokana na joto la chini.
Kunguni/mende mwembamba wa mpunga hushambulia mpunga na mazao mengine, kama vile soya. Majike hutaga mayai moja baada ya nyingine kwenye majani ya mpunga. Kunguni wachanga wa kwanza huanguliwa ndani ya siku 7 hivi. Wanakua kupitia hatua tano kabla ya kugeuka kuwa wadudu wazima. Kunguni/mende wadogo hufanana na wakubwa japo kimwonekano ni wadogo zaidi. Wakati wa majira ya baridi yasiyo na baridi kali, kiasi kikubwa cha mende hawa huishi. Kwa hiyo, katika miaka ambayo haina baridi kali, unaweza kuwaona zaidi.