Acherontia styx
Mdudu
Viwavi/funza hula majani machanga na mashina yanayokua, na kutengeneza mashimo/matobo yanayoonekana na uharibifu wa nje kwenye majani. Ukichunguza mmea kwa karibu, unaweza kuona viwavi wa kijani au kahawia.
Ili kudhibiti uvamizi wa nondo mwewe, kunyunyizia Kerneli ya Mbegu ya Mwarobaini (NSKE) kunaweza kuwa njia nzuri. NSKE ni dawa ya asili inayotokana na mbegu za mwarobaini na inajulikana kwa uwezo wake wa kuzuia wadudu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na nondo mwewe. Kwa kuwa hawa ni wadudu wasio na madhara makubwa unaweza kuondoa viwavi kwa mikono kutoka kwenye majani, njia ambayo inafaa katika maeneo madogo.
Kwa kuwa huyu ni mdudu mwenye madhara madogo, ni bora kutumia mbinu za udhibiti ambazo ni rafiki kwa mazingira pamoja na hatua za kuzuia. Ikiwa idadi ya yao tayari imeongezeka na udhibiti wa kemikali unahitajika, inashauriwa kutumia Quinalphos. Unapotumia dawa za wadudu au bidhaa yoyote ya kemikali, ni muhimu kuvaa nguo za kujikinga na kusoma kwa uangalifu maagizo ya lebo. Kanuni hutofautiana kulingana na nchi, kwa hivyo hakikisha unafuata miongozo mahususi ya eneo lako. Hii inahakikisha usalama na huongeza nafasi za matumizi yenye ufanisi.
Uharibifu huo unasababishwa na ulaji wa viwavi/funza wa nondo. Kiwavi/funza huyo ni mnene na imara mwenye mwili wa kijani na mistari ya pembe . Wana mwiba unaoonekana kama ndoano mgongoni mwao. Nondo mwewe mkubwa ana rangi ya kahawia na alama maalum ya fuvu kwenye kifua chake. Ana michirizi ya urujuani na njano kwenye tumbo lake na mabawa yake ni kahawia iliyokolea na manjano yenye mistari myeusi.