Xanthodes transversa
Mdudu
Viwavi hula kwenye majani na kusababisha kupukutika kwa majani. Ulaji majani huvuruga usanisinuru(photosynthesis) na matokeo yake ukuaji na uzalishaji wa mazao huathiriwa vibaya.
Udhibiti wa kibayolojia haupo kwa mdudu huyu mdogo. Ikiwa inahitajika, waondoe kwa mkono.
Ikiwa kuna viwavi wengi katika hatua ya awali ya ukuaji, inaweza kuwa muhimu kuchukua hatua ili kuzuia uharibifu. Unapaswa kuchukua hatua haraka mara tu unapoona dalili za uharibifu. Katika mashamba makubwa ambayo yanakuza bamia ili kuuza nje ya nchi, viwavi wengi katika hatua ya awali wanaweza kusababisha madhara ya kiuchumi. Unapaswa kuwasiliana na mtaalamu wa kilimo kwa ushauri juu ya bidhaa za kutumia, na uhakikishe kufuata kanuni unapotumia viua wadudu.
Uharibifu husababishwa na Xanthodes transversa, nondo. Hula mazao kadhaa muhimu kiuchumi ambayo mengi ni mimea ya familia ya Malvaceae. Majike hutaga mayai yao kwenye sehemu ya chini ya majani moja baada ya jingine. Viwavi wadogo hutoka kwenye mayai baada ya wiki. Kiwavi aliyekua kikamilifu ana rangi ya kijani kibichi na mstari wa manjano wa kipekee mgongoni ulio sambamba na urefu wa mwili (kutoka mkiani hadi kichwani) na alama za rangi nyeusi zenye umbo la kwato ya farasi kwenye pande zote za mstari wa manjano. Katika hatua za baadaye kiwavi ana mwonekano tofauti kidogo aa rangi. Lava wachanga ni kama nyuzi na huzunguka sana. Wanakula chini ya majani, ambapo wanaweza pia kupatikana. Viwavi hujificha kwenye udongo na kujigeuza kuwa pupa na nondo hutoka baada ya wiki kadhaa. Nondo waliokomaa ni wa manjano, wakiwa na mistari mitatu ya kahawia yenye umbo la mishale katika kila ubawa wa mbele. Vipindi vya hali ya hewa ya joto na unyevu husaidia mdudu huyu. Ingawa haleti uharibifu mkubwa, bado anaweza kudhuru mazao.