Mzeituni

Kome wa Zambarau

Lepidosaphes beckii

Mdudu

Kwa Ufupi

  • Wadudu wa mviringo, bapa, wa kahawia-zambarau wanaofanana na matuta madogo kwenye sehemu za mimea.
  • Madoa ya kijani kwenye matunda ambapo wadudu hula.

Inaweza pia kupatikana kwenye


Mzeituni

Dalili

Kome wa zambarau hushikamana na nyuso za mimea, hasa matunda, majani, matawi na shina. Wanakula kwenye majimaji ya mmea, ambayo hasababisha madhara kadhaa yanayoonekana. Matunda yaliyoiva huanza kugeuka kijani hafifu mahali ambapo kome hula. Majani yanageuka manjano na yanaweza kudondoka kutoka kwenye mmea. Katika hali mbaya, ncha za matawi zinaweza kuanza kufa na uharibifu huu unaweza kuenea kwa kurudi nyuma kuelekea sehemu kuu ya matawi.

Mapendekezo

Udhibiti wa Kiasili

Nyunyiza miti kwa mafuta bwete na salfa ya chokaa mwishoni mwa msimu wa baridi kabla ya mayai ya kwanza kuanguliwa au ukigundua kushambuliwa mapema. Kwa miti midogo, au sehemu zinazoweza kufikiwa za miti mikubwa, unaweza kusugua magamba kwa kutumia kisusulo cha sahani za plastiki. Kwa kawaida, maadui wa asili huzuia idadi ya wadudu hawa, kwa hivyo huwa si tatizo kubwa.

Udhibiti wa Kemikali

Mdudu huyu kwa kawaida husababisha uharibifu mdogo, lakini kwa idadi kubwa, anaweza kusababisha madhara makubwa, ambayo yanaweza kuhitaji udhibiti wa kemikali. Wadudu hawa ni wagumu kuua kwa dawa mara tu unapowagundua kwa sababu magamba yao magumu huwalinda. Njia bora ya kuwadhibiti ni kuwatibu mapema katika msimu ambapo wadudu wachanga wasiolindwa wanazunguka kabla hawajatulia kula. Ni vyema kuepuka kutumia viua wadudu vikali, vya wigo mpana, kama vile pyrethroid ya kiwandani, kwa sababu vinaweza kuua wadudu hawa wenye manufaa. Pendelea kutumia viua wadudu vinavyoweza kufyonzwa na mmea.

Ni nini kilisababisha?

Vinundu kwenye mmea wako ni magamba ya kome wa zambarau wa kike. Hawatembei na hujificha chini ya kifuniko cha kinga cha rangi ya kahawia-zambarau. Jike hutaga mayai chini ya gamba lake la kinga, ambapo hukaa salama wakati wa majira ya baridi na huanguliwa mwishoni mwa Mei au Juni. Wadudu hawa huzaa mara moja kwa mwaka. Wadudu wadogo wanaweza kutembea na kuenea kwenye mimea mipya kwa kutembea au kubebwa na upepo, magari, wanyama, ndege, na nguo za watu. Wanaweza pia kuenea kupitia nyenzo za mimea ambazo hubeba wadudu juu yao.


Hatua za Kuzuia

  • Tumia nyenzo zisizo na wadudu.
  • Weka mimea yenye afya kwa kuipatia maji ya kutosha na lishe huisaidia kuzuia wadudu.
  • Ukaguzi wa mara kwa mara wa wadudu -gamba kwenye bustani ni muhimu.
  • Usisahau kuangalia upande wa chini wa majani au mashina machanga kwa wadudu wakubwa, haswa kwenye madoa yenye kivuli au yaliyo funikwa.
  • Utambuzi wa mapema ni muhimu! Ingawa unaweza kuona wadudu wazima kwa jicho tupu, wadudu wachanga ni vigumu kuwaona.
  • Ili kugundua kizazi cha kwanza cha wadudu wachanga, funga mkanda wa kunata wa pande mbili kwenye matawi ya miti ambayo hapo awali yalikuwa yamevamiwa.
  • Wadudu wachanga ni wadogo, bapa, angavu, na miguu myembamba.
  • Angalia mkanda kila siku ili kuona ikiwa wadudu wadogo wame nata.
  • Ikiwa mkanda unapata mvua au vumbi, ubadilishe.
  • Vinginevyo, unaweza kushikilia kipande cha karatasi nyeupe chini ya matawi na kuyapiga kwa fimbo.
  • Wadudu watambaao, ambao wanaweza kuwa weupe, njano, machungwa, au zambarau, wataanguka na kuonekana wazi kwenye karatasi nyeupe.

Pakua Plantix