Lepidosaphes beckii
Mdudu
Kome wa zambarau hushikamana na nyuso za mimea, hasa matunda, majani, matawi na shina. Wanakula kwenye majimaji ya mmea, ambayo hasababisha madhara kadhaa yanayoonekana. Matunda yaliyoiva huanza kugeuka kijani hafifu mahali ambapo kome hula. Majani yanageuka manjano na yanaweza kudondoka kutoka kwenye mmea. Katika hali mbaya, ncha za matawi zinaweza kuanza kufa na uharibifu huu unaweza kuenea kwa kurudi nyuma kuelekea sehemu kuu ya matawi.
Nyunyiza miti kwa mafuta bwete na salfa ya chokaa mwishoni mwa msimu wa baridi kabla ya mayai ya kwanza kuanguliwa au ukigundua kushambuliwa mapema. Kwa miti midogo, au sehemu zinazoweza kufikiwa za miti mikubwa, unaweza kusugua magamba kwa kutumia kisusulo cha sahani za plastiki. Kwa kawaida, maadui wa asili huzuia idadi ya wadudu hawa, kwa hivyo huwa si tatizo kubwa.
Mdudu huyu kwa kawaida husababisha uharibifu mdogo, lakini kwa idadi kubwa, anaweza kusababisha madhara makubwa, ambayo yanaweza kuhitaji udhibiti wa kemikali. Wadudu hawa ni wagumu kuua kwa dawa mara tu unapowagundua kwa sababu magamba yao magumu huwalinda. Njia bora ya kuwadhibiti ni kuwatibu mapema katika msimu ambapo wadudu wachanga wasiolindwa wanazunguka kabla hawajatulia kula. Ni vyema kuepuka kutumia viua wadudu vikali, vya wigo mpana, kama vile pyrethroid ya kiwandani, kwa sababu vinaweza kuua wadudu hawa wenye manufaa. Pendelea kutumia viua wadudu vinavyoweza kufyonzwa na mmea.
Vinundu kwenye mmea wako ni magamba ya kome wa zambarau wa kike. Hawatembei na hujificha chini ya kifuniko cha kinga cha rangi ya kahawia-zambarau. Jike hutaga mayai chini ya gamba lake la kinga, ambapo hukaa salama wakati wa majira ya baridi na huanguliwa mwishoni mwa Mei au Juni. Wadudu hawa huzaa mara moja kwa mwaka. Wadudu wadogo wanaweza kutembea na kuenea kwenye mimea mipya kwa kutembea au kubebwa na upepo, magari, wanyama, ndege, na nguo za watu. Wanaweza pia kuenea kupitia nyenzo za mimea ambazo hubeba wadudu juu yao.