Pseudomonas syringae pv. tabaci
Bakteria
Dalili zinaweza kutokea kwa haraka. Madoa huonekana hasa kwenye majani lakini pia yanaweza kutokea kwenye mashina, maua, na kapsuli za matunda ya tumbaku. Mado kawaida huzungukwa na halo ya manjano. Madoa huanza kama sehemu ndogo za duara za kijani hafifu, ambazo hubadilika kuwa kahawia katikati kutokana na kufa kwa tishu. Madoa yanaweza kuungana. Katika hali mbaya, sehemu zilizoharibiwa za majani huanguka, na mishipa ya majani tu huachwa. Moto wa nyika unaweza kuathiri mazao katika hatua yoyote ya ukuaji, ikiwa ni pamoja na miche kwenye kitalu.
Chaguzi mbadala za udhibiti wa moto wa nyika hutegemea zaidi matumizi ya hatua za kuzuia na mazoea mazuri ya shughuli za shambani.
Kudhibiti vimelea hawa kunaweza kuhusisha matumizi ya kemikali zenye msingi wa shaba, kama mchanganyiko wa Bordeaux, wakati wa hatua za awali za ukuaji wa mmea. Katika maeneo ambayo matumizi ya kilimo yameidhinishwa, dawa ya streptomycin inaweza kuchukuliwa kuwa mbadala. Hata hivyo, ufanisi wa streptomycin unaweza kuathiriwa kwani bakteria wanaweza kutengeneza ukinzani dhidi yake kwa haraka. Unapotumia dawa za wadudu au bidhaa yoyote ya kemikali, ni muhimu kuvaa nguo za kinga na kusoma kwa uangalifu maagizo ya lebo. Kanuni hutofautiana kulingana na nchi, kwa hiyo hakikisha unafuata miongozo mahususi ya eneo lako. Hii inahakikisha usalama na huongeza nafasi za matumizi yenye mafanikio.
Bakteria anaesababisha ugonjwa hustawi katika hali ya joto na unyevunyevu, mara nyingi huenea baada ya dhoruba za mvua. Upepo una jukumu kubwa katika jnamna na wapi ugonjwa utaenda. Kumwagilia mimea kwa vinyunyiziaji kunaweza pia kueneza bakteria kwa njia sawa. Bakteria anaweza kuingia kwenye mimea ya tumbaku kupitia fursa za asili au majeraha ya wadudu. Mara tu akiingia ndani, bakteria hukua na kuenea ndani ya mmea. Mmea unapoanza kuoza na kufa, bakteria hutolewa tena kwenye mazingira, ambapo anaweza kuambukiza mimea mingine au kukaa kwenye udongo kwa muda wa miaka miwili. Bakteria pia anaweza kuhamia maeneo mapya kupitia taka za mimea iliyoambukizwa, udongo, au zana za kilimo.