Glomerella cingulata
Kuvu
Kuvu husababisha dalili mbalimbali, kulingana na tishu zilizoshambuliwa na hali ya hewa. Madoa madogo sana yaliyozama ya rangi mbalimbali huonekana kwenye majani, shina, maua au matunda, mara nyingi yakiwa yamezungukwa na mduara angavu wa njano wenye alama zaidi au kiasi. Kwenye majani, madoa huongezeka baadaye na kuunda vidonda na yanaweza kufunika sehemu kubwa ya ubapa wa jani. Yanageuka njano na yanaweza kuanguka mapema na kusababisha kupukutika kwa majani. Madoa kwenye matunda yana rangi ya kahawia hadi kahawia iliyokolea, kwanza ni ya mviringo, kisha yanakuwa hayana umbo maalumu kadri yanavyopanuka. Tunda hilo baadaye hulainika na kuoza hutokea kwenye arili ambazo hubadilika kuwa kijivu iliyokolea au nyeusi lakini hazina maji. Chule pia inaweza kushambulia vijitawi na matawi na kusababisha uvimbe/vikwachu, ambayo ni maeneo ya tishu zilizozama, zilizoambukizwa na kingo zilizovimba. Maambukizi ya shina mara chache yanaweza kusababisha mguguno unao kwamisha maji navirutubisho visipite na kufa
Mawakala wa udhibiti wa kibayolojia wanaojulikana ni fangasi washindani Aspergillus flavus, Hypocrea rufa, Hyponectria tuberculariformis, na Nectriella muelleri. Wa kwanza tu ndiye mpinzani wa kweli. Wengine ni wanyonyaji au vimelea wa magonjwa.
Daima zingatia mbinu jumuishi na hatua za kuzuia pamoja na matibabu ya kibayolojia ikiwa yanapatikana. Dawa ya kwanza ya kuzuia inaweza kunyunyiziwa wakati maua yanaanza na hali za kimazingira zikiwa nzuri kwa kuvu. Kisha nyunyiza kwa muda wa siku 15 mara mbili, ikiwa ni lazima. Viambata hai vinavyotumika ni propiconazole, mancozeb au mchanganyiko wa mancozeb na tricyclazole. Nyunyiza dawa za kuua kuvu tu zenye usajili halisi kwajili ya komamanga. Ni muhimu kufuata viwango vilivyoainishwa na kutumia dawa za kuua kuvu zenye muundo tofauti wa ufanyaji kazi ili kuzuia ukinzani/usugu.
Dalili husababishwa na fangasi Glomerella cingulata. Huishi katika mabaki ya mimea iliyoambukizwa kwenye uso wa udongo au katika matunda yaliyokaushwa. Katika majira ya kuchipua, vijimbegu vyake huenezwa kupitia mvua au upepo na huambukiza matawi au mimea ya jirani. Hatua zinazoathirika zaidi ni kipindi cha maua na ukuaji wa matunda. Majeraha kutokana na miiba ya miti, wadudu, na wanyama huchochea mchakato wa kuambukizwa. Mvua za mara kwa mara, unyevu mwingi (50-80%) na kiwango cha joto cha 25-30°C ni rafiki kwa mzunguko wa maisha ya kuvu. Hata hivyo, kwa kawaida kuvu huwa bwete katika msimu wa kiangazi. Hata madhara ya mwanga yanaweza kusababisha uharibifu wa uzuri/mvuto wa matunda na kufupisha mda wake wa kuhifadhi. Mimea mingine inashoshambuliwa ni kwa mfano Maembe, Mapera na Papai.