Matunzo
Pilipili hoho au hoho ni mmea unaotoa maua wa familia ya nightshade. Asili yake inatokea Americas (masalia ya kilimo chake yalipatikana Meksiko mnamo 3,000 KK) na ulitambulishwa kwingineko duniani baada ya karne ya 16. 50% ya pilipili hoho zote kwa sasa hupandwa nchini China, ikifuatiwa na Meksiko, Uturuki, Indonesia na Uhispania.
Udongo
Pilipili hoho inaweza kulimwa kwenye aina nyingi za udongo lakini hukua vyema kwenye udongo wenye kina kirefu, tifutifu na usiotuamisha maji. pH ya udongo inapaswa kuwa kati ya 5.5-7.0. Zinaweza kuunda mizizi imara yenye kina kirefu (> mita 1 ). Miteremko inayoshuka kwa usawa hufaa, kwani husaidia kupitisha maji vizuri, lakini sio lazima. Mabonde shambani yanaweza kusababisha mafuriko.
Hali ya hewa
Hali zinazofaa zaidi kwenye kilimo cha pilipili hoho ni pamoja na mahali penye jua na udongo tifutifu wa vuguvugu, wa 21°C hadi 29°C, wenye unyevunyevu lakini usiojaa maji. Udongo wenye unyevunyevu kupita kiasi unaweza kusababisha miche "kufa" na kupunguza uchipuaji. Mimea itastahimili (lakini haipendelei) joto la hadi kufikia 12 °C na huathiriwa kiurahisi na jalidi. Utoaji maua wa Hoho huhusiana sana na urefu wa siku. Maua yanaweza kujichavusha yenyewe. Hata hivyo, katika halijoto ya juu sana (33°C hadi 38°C), chavua hupoteza uwezo wake wa kumea, na maua huwa na uwezekano mdogo sana wa kuchavusha kwa mafanikio.