Matunzo
Bamia (Abelmoschus esculentus) ijulikanayo pia kama 'ladies fingers' hulimwa kote duniani katika maeneo ya tropiki na yenye halijoto ya vuguvugu. Huthaminiwa kwa maganda yake ya mbegu, ambayo huweza kuliwa pindi yanapokuwa machanga. Ngozi kavu ya matunda na nyuzinyuzi hutumiwa katika utengenezaji wa karatasi, kadibodi na nyuzi. Mizizi na shina hutumiwa kusafisha maji ya miwa kwa ajili ya uandaaji wa sukari guru.
Udongo
Bamia inaweza kuoteshwa katika aina mbalimbali za udongo. Hustawi vizuri zaidi kwenye udongo wa michanga wenye rotuba, uliolegea, unaopukutika, na usiotuamisha maji, wenye maada ya kikaboni ya kutosha. Inaweza pia kutoa mazao mazuri kwenye udongo mzito ili mradi tu udongo huo uweze kupitisha maji kwa urahisi. pH bora kwa mmea huu ni kati ya 6.0-6.8. Udongo wa alkali, chumvi na udongo unaotuamisha maji sio mzuri kwa zao hili.
Hali ya hewa
Bamia ni mojawapo ya mboga zinazostahimili joto na ukame duniani; ikishapandwa, inaweza kustahimili hali mbaya za ukame. Hata hivyo, Bamia hukua vyema zaidi katika hali za uvuguvugu na unyevunyevu, zenye halijoto ya kati ya 24-27°C.