Matunzo
Embe lina umuhimu mkubwa kiuchumi na linapendwa na walaji kutokana na ladha yake nzuri na aina zake mbalimbali. Lina virutubishi vingi vya vitamini A na C. Mti wa mwembe pia unaweza kutumika kama mbao na kwa madhumuni ya kidini. Majani yanaweza kulishwa kwa mifugo kama chakula.
Udongo
Embe linaweza kufanikiwa kukua kwenye aina mbalimbali za udongo, huku udongo tifutifu mwekundu ukiwa ndio bora zaidi. Udongo unapaswa kuwa na uwezo mzuri wa kuhifadhi maji, lakini udongo usioweza kupitisha maji kwa urahisi utazuia ukuaji. Udongo wa aluvia wa kina (zaidi ya 1.2m), wenye maada za kikaboni utawezesha ukuaji bora. Kwa sababu hizi, kulima kwenye tambarare badala ya milimani kunapendekezwa.
Hali ya hewa
Embe hukua vizuri katika maeneo mengi ya tropiki na ya tropiki ya kati lakini huathiriwa kiurahisi na joto kali na jalidi. Unyeshaji wa mvua wa viwango tofauti-tofauti katika hatua za upandaji mazao ni muhimu katika kuwezesha mavuno yenye mafanikio. Kwa mfano, hali ya hewa kavu ni nzuri kwa ajili ya uchavushaji utokeao wakati wa uchepuaji wa maua, huku hali ya hewa ya mvua ikisaidia kwenye uzalishaji wa matunda. Upepo mkali unaweza kuharibu miti ya miembe.