Matunzo
Biringanya, inayojulikana pia kama biringani, ni mmea wa familia ya nightshade (Solanaceae) na hupandwa kwa ajili ya matunda yake yanayoliwa. Zao hili hapo awali lililimwa nchini India na sasa linaweza kupatikana katika tabia nchi zenye hali ya hewa ya vuguvugu duniani kote.
Udongo
Solanum melongena huhitaji udongo wenye rutuba, wenye matundu matundu, unaopitisha maji kwa urahisi lakini usio mkavu. Udongo unapaswa kuwa na asidi kidogo tu, pH ya 6.5 hufaa zaidi. Mizizi ya mmea huu huingia hadi umbali wa sm 50 ndani ya udongo, kwa hiyo udongo usio na kizuizi hupendelewa zaidi.
Hali ya hewa
Solanum melongena hukua katika tabia nchi za kitropiki hadi za joto la wastani. Inapooteshwa katika hali ya hewa za baridi hatua za ukuaji hubidi kuanzia katika nyumba ya uoteshaji mimea kwanza mpaka pale udongo utakapokua na joto la kutosha kuruhusu upandikizaji. Katika tabia nchi za baridi zao hili hupandwa kama zao la kila mwaka, wakati tabia nchi za vuguvugu huruhusu upandaji wa kudumu. Mwanga wa jua wa moja kwa moja huwa na faida kwenye ukuaji wa mmea.