Matunzo
Miti jamii ya mchungwa ni jamii ya miti inayochanua maua na vichaka katika familia ya Rutaceae, asili yake inatokea maeneo ya tropiki ya kati na ya kitropiki ya kusini-Mashariki mwa Asia. Leo, spishi zingine ni muhimu kiuchumi katika bonde la Mediterania, bara la India na kusini mwa USA, ambapo hupata udongo pamoja na hali ya hewa nzuri. Machungwa, malimao, balungi, na ndimu ni miongoni mwa matunda ya miti ya jamii ya mchungwa.
Udongo
Miti ya jamii ya mchungwa huhitaji kati ya sm 60 na mita 1 ya udongo wa juu unaoweza kupitisha maji vizuri ili kukua vyema. Udongo tifutifu na michanga tifutifu hupendekezwa, uongezaji mboji pia hufaa zaidi. Katika udongo wenye mchanga mwingi, wenye uwezo mdogo wa kuhifadhi maji, kuna hatari ya virutubisho kupotea. Udongo wa mfinyanzi unaweza kusababisha kuoza kwa kola na mizizi na hata hatari ya mti kufa. pH bora ni kati ya 6.0 na 6.5 na pH zaidi ya 8 inapaswa kuepukwa. Miteremko ya hadi 15% inafaa ikiwa kama mmomonyoko wa udongo na utiririshaji wa maji kupita kiasi vitaepukwa. Vizuia upepo vinapendekezwa
Hali ya hewa
Spishi hizi hufurahia zaidi maeneo ya uvuguvugu yenye halijoto ya wastani lakini zina uwezo wa kustahimili baridi kali (kutegemeana na aina). Jamii ya mchungwa huweza kustahimili joto la juu ikiwa kama unyevu wa udongo ni bora. Miti ina uwezo wa kustahimili baridi kali lakini kwa ujumla haipendekezwi katika maeneo yenye jalidi kali za mara kwa mara. Upinzani dhidi ya baridi hutofautiana baina ya aina ya mti, umri wa miti na afya ya mti. Mti mchanga utaharibiwa hata na theluji nyepesi ilhali mti uliokomaa unaweza kustahimili halijoto ya hadi -5° C kwa muda mfupi. Miti iliyo na shida ni rahisi zaidi kuathiriwa.