Matunzo
Ndizi ni tunda linaloweza kuliwa, linalozalishwa na aina kadhaa za mimea mikubwa inayotoa maua katika jamii ya Musa. Baadhi ya ndizi hutumiwa kupikwa, nyingine huliwa kama matunda (kitindamlo). Asili ya Spishi za Musa ni huko Asia ya Kusini-mashariki na Australia. Ndizi kimsingi ni zao la tropiki, ambalo hupendelea maeneo ya chini yenye unyevunyevu, lakini linaweza kulimwa kutoka usawa wa bahari hadi kwenye mwinuko wa mita 2000.
Udongo
Migomba itakua kwenye aina nyingi za udongo, lakini ili istawi vizuri zaidi, inapaswa ipandwe kwenye udongo wenye rutuba, wenye kina kirefu, usiotuamisha maji, ambao unaweza kuwa tifutifu wa msituni, mchanga wa miamba, maga, ngegu mwekundu, majivu ya volkano, mfinyanzi wa michanga au mfinyanzi mzito. Hupendelea udongo wenye asidi na pH ya kati ya 5.5 na 6.5. Ndizi haistahimili udongo wenye chumvi nyingi. Kipengele muhimu cha aina ya udongo kinachofanikisha ukuaji mzuri wa migomba ni upitishaji maji. Udongo uliopo kando ya mabonde ya mito ni bora zaidi kwa ajili ya uoteshaji wa ndizi.
Hali ya hewa
Migomba huhitaji miezi 10 - 15 ya hali isiyo na ubaridi yenye joto la 15-35°C ili kutoa shina la ua. Aina nyingi huacha kukua pale halijoto inaposhuka chini ya 53°F (11.5 °C). Kuelekea viwango vya juu vya joto, ukuaji hupungua katika takriban 80°F (26,5 °C) na husimama kabisa halijoto inapofikia 100°F (38°C). Halijoto ya juu na jua kali vinaweza kuunguza majani na matunda, ingawa ndizi hukua vyema kwenye jua. Baridi kali litaua majani. Ndizi huwa rahisi kupeperushwa na upepo.