Matunzo
Tofaa ni tunda linalokua katika hali ya hewa ya wastani ambalo huliwa kama lilivyo, huku asilimia ndogo ya uzalishaji wake ikitumika kwa ajili ya bidhaa za makopo na nyinginezo zinazochakatwa. Tofaa ni tunda la nne linalozalishwa zaidi duniani.
Udongo
Udongo wa tifutifu, usiotuamisha maji wenye pH ya 5.5-6.5 ni bora kwa uzalishaji wa tofaa. Udongo haupaswi kuwa umejaa maji au kuwa na udongo wa chini ulioshikamana. Matandazo yaliyochanganywa na vitu vya kikaboni yanaweza kusaidia kuhifadhi unyevu wa udongo.
Hali ya hewa
Tofaa ni zao linalokua katika hali ya hewa ya wastani na hustawi katika halijoto ya kati ya 21 na 24 selisiasi. Matunda haya yanaweza pia kukuzwa katika miinuko ya juu (m 1500-2700 juu ya usawa wa bahari). Mvua inayosambaa sawasawa katika msimu wote wa ukuaji ni bora katika kuwezesha ukuaji wa tofaa. Hali ya upepo ni hatari kwa miti ya tofaa. Hali kavu, ya jua husaidia kuzalisha matunda yenye sukari nyingi na yawezayo kudumu kwa muda mrefu.